Picha mbalimbali za matukio ya mahafali ya kidato cha sita 2019 yaliyofanyika tarehe 06.05.2019 shuleni Eagles. Waliovalia fulana ni wahitimu wa kidato sita wakifurahia siku hii muhimu.
Meneja wa Sekondari ya Eagles Bw George Fumbuka akizungumza na wahitimu siku ya mahafali ya Form VI 2019
Mkuu wa Sekondari ya Eagles Bw Myombe Adam Mgonde akihutupia kwenye mahafali ya Form VI 2019
Wahitimu wakionyesha michezo mbalimbali kwenye mahafali
Mgeni wa heshimma akisalimia na walimu wa sekondari ya Eagles
Gwaride la ukakamavu. Wanafunzi wameshiriki kwenye Gwaride ikiwa ni utaratibu wa kila siku ya Jumamosi. Utaratibu huo una lengo la kujenga afya ya mwili na akili, kujenga uzalendo na ukakamavu kwa ujumla.
Wanafunzi wanaosoma masomo ya biashara wakimsikiliza Mkurugenzi Bw George Fumbuka akifundisha mada ya mbalimbali za kiuhasibu. Kwenye picha anaonekana akifundisha kwa kutumia njia shirikishi ambapo wanafunzi wameshiriki moja kwa moja. Pia kwenye darasa hili wapo walimu wa masomo ya biashara.
Wanafunzi wanaosoma somo la Kifaransa wakiwa kwenye picha tofauti na walimu wao tarehe 15.03.2019 katika chuo kikuu kishiriki cha elimu DUCE. Wanafunzi hao walifanya ziara hiyo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Kifaransa.
MUHIMU: Shule ya Eagles imeanza kufundisha somo la Kifaransa kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne na comb ya KLF kwa kidato cha tano na cha sita.