Picha mbalimbali za matukio ya mahafali ya kidato cha sita 2019 yaliyofanyika tarehe 06.05.2019 shuleni Eagles. Waliovalia fulana ni wahitimu wa kidato sita wakifurahia siku hii muhimu.

mahafari kidato cha sita 06 05 2019 09

Meneja wa Sekondari ya Eagles Bw George Fumbuka akizungumza na wahitimu siku ya mahafali ya Form VI 2019

 

mahafari kidato cha sita 06 05 2019 092

Mkuu wa Sekondari ya Eagles Bw Myombe Adam Mgonde akihutupia kwenye mahafali ya Form VI 2019

 

mahafari kidato cha sita 06 05 2019 094

Wahitimu wakionyesha michezo mbalimbali kwenye mahafali

 

mahafari kidato cha sita 06 05 2019 095

Mgeni wa heshimma akisalimia na walimu wa sekondari ya Eagles



morning parade
Gwaride la ukakamavu. Wanafunzi wameshiriki kwenye Gwaride ikiwa ni utaratibu wa kila siku ya Jumamosi. Utaratibu huo una lengo la kujenga afya ya mwili na akili, kujenga uzalendo na ukakamavu kwa ujumla.


 mkurugenzi akifundish uhasibu 2019 03 30

Wanafunzi wanaosoma masomo ya biashara wakimsikiliza Mkurugenzi Bw George Fumbuka akifundisha mada ya  mbalimbali za kiuhasibu. Kwenye picha anaonekana akifundisha kwa kutumia njia shirikishi ambapo wanafunzi wameshiriki moja kwa moja. Pia kwenye darasa hili wapo walimu wa masomo ya biashara.


 ziarani duse 2019 03 16 at 13.51.01


Wanafunzi wanaosoma somo la Kifaransa wakiwa kwenye picha tofauti na walimu wao tarehe 15.03.2019 katika chuo kikuu kishiriki cha elimu DUCE. Wanafunzi hao walifanya ziara hiyo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Kifaransa.
MUHIMU: Shule ya Eagles imeanza kufundisha somo la Kifaransa kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne na comb ya KLF kwa kidato cha tano na cha sita.