Tarehe 7 Machi 2020 kwenye shule ya sekondari ya Eagles kulifanyika mkutano wa wazazi, wafanyakazi pamoja na viongozi wa shule. Lengo la mkutano huu ni kujadili mambo mbalimbali yanayohusu shule ikiwa ni pamoja na maendeleo ya taaluma, nidhamu na ustawi wa wanafunzi. Mkutano umekuwa mzuri na umeleta matokeo chanya.