Jumatatu tarehe 1.05.2020 walimu wa Eagles High School walifanya semina kwa wanafunzi wa kidato cha sita kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kujiandaa na mtihani wao wa taifa huku wakichukua tahadhari ya ugonjwa wa Covid-19.
Mambo mengi yalizungumzwa ikiwa ni pamoja na kuondoa hofu ya mtihani, kujiamini, kujisomea kwa njia ya mjadala (group discussion), kumtanguliza Mungu na kutumia muda huu vizuri kufanya maandalizi. Hayo yameelezwa huku kila mmoja akisisitizwa kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa mapafu.
Tarehe 7 Machi 2020 kwenye shule ya sekondari ya Eagles kulifanyika mkutano wa wazazi, wafanyakazi pamoja na viongozi wa shule. Lengo la mkutano huu ni kujadili mambo mbalimbali yanayohusu shule ikiwa ni pamoja na maendeleo ya taaluma, nidhamu na ustawi wa wanafunzi. Mkutano umekuwa mzuri na umeleta matokeo chanya.