Baraza la mitihani la Taifa ( NECTA) limetoa matokeo ya kidato kidato cha pili na cha nne.
Kwa kidato cha pili: ftna_results_S2354-2019.pdf
Div:I- 09
II-14
III- 04
IV- 03
Hakuna div 0.
Kwa kidato cha nne: csee_results_s2354-2019.pdf
Div: I- 17
II- 46
III- 14
IV- 02
Hakuna div 0.
Wanafunzi 77 waliomaliza kidato cha nne wanna sifa ya kujiunga kidato cha tano mwaka huu huku wanafunzi 02 wakiwa wamepata div 4 ya point 26 ambayo wanaweza kupata nafasi ya kujiunga na vyuo mbalimbali.
Mahafari hiyo ilifanyika tarehe 19/10/2019 na kuhudhuriwa na wazazi, watumishi pamoja na wageni mbalimbali. Pia mahafari ilihudhuriwa na wajumbe wa bodi ya shule wakiongoza na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Mama Eva Fumbuka.
Mgeni rasmi kwenye mahafari hii alikuwa Ndg. Kwangu Masalu Zabrone ambaye ni kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Utafiti na Machapisho wa Taasisi ya Elimu. Yeye alimwakilisha Mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Dkt. Aneth Komba ambaye ndiye alitarajiwa kuwepo kwenye mahafari hiyo.
Katika mahafari hii kulifanyika pia maonesho ya kitaaluma (Academic exhibitions) ambayo yalikuwa kivutio kikubwa kwa wazazi pamoja na wageni mbalimbali.
Eagles ni shule ya sekondari ya wavulana, wote bweni, yenye Kidato cha 1 hadi cha 6. Imesajiliwa kama shule binafsi kwa namba S.2397 mwaka 2006 kutoa elimu ya sekondari kwa mitaala ya Tanzania. Shule yetu iko umbali wa kilometa 2 kutoka kituo kipya cha mabasi cha Bagamoyo karibu na kanisa kongwe Katoliki na Chuo cha ADEM upande wa magharibi.
MWAKA |
DIVISION I |
DIVISION II |
DIVISION III |
DIVISION IV / ZERO |
2015 |
4 |
5 |
11 |
0 |
2016 |
11 |
29 |
23 |
0 |
2017 |
7 |
35 |
54 |
0 |
2018 |
16 |
40 |
24 |
0 |
2019 |
16 |
56 |
36 |
0 |
Shule ina mazingira mazuri ya kitaaluma, walimu wa kutosha wenye sifa na mikakati mizuri ya kitaaluma yenye lengo la kumwezesha mwanafunzi kufaulu masomo yake. Aidha, Shule imeanzisha mfumo wa kufundisha kwa kutumia iPads za Apple zilizounganishwa na mtandao (Internet) ikiwa ni mkakati wa kuboresha ufundishaji ili uendane na teknolojia ya mawasiliano. Shule inayo masomo yote ya Sayansi, Sanaa, Biashara, Kilimo, Lugha na Kompyuta. Kwa Kidato cha 5 na cha 6 shule ina tahsusi zifuatazo:
Sanaa/Lugha: HGL (History, Geography, (English) Language); HGK (History, Geography, Kiswahili), HKL (History, Kiswahili, Language); KLF (Kiswahili, Language, French)
Biashara: ECA (Economics, Commerce, Accountancy); EGM (Economics, Geography, Mathematics); HGE (History, Geography, Economics); AgBE (Agriculture, Biology, Economics)
Sayansi: PCM (Physics, Chemistry, Mathematics); PCB (Physics, Chemistry, Biology); CBG (Physics, Biology, Geography); PMCs (Physics, Mathematics, Computer Science); CBCs (Chemistry, Biology, Computer Science); PCsG (Physics, Computer Science, Geography); PGM (Physics, Geography, Mathematics), CBA (Chemistry, Biology, Agriculture).
Shule ya sekondari Eagles imeanzisha mfumo wa kufundisha kwa kutumia iPad zilizounganishwa na internet. Mfumo huu unatajwa kuwa na manufaa mengi zaidi ikiwa ni pamoja na kumfanya mwanafunzi kulipenda somo hivyo kuongeza ufaulu. Pia mfumo huu unamuwezesha mwalimu kufundisha kwa kutumia mbinu shirikishi.
Kwa mala nyingine shule ya sekondari ya Eagles imeshiriki kwenye mbio za Bagamoyo Marathon 2019. Mwaka huu watumishi wameshiriki kwa wingi zaidi ya mwaka jana. Lengo kubwa la mbio hizo ni kujenga umoja, kuimalisha afya ya watumishi, lakini kipekee sana ni kuitangaza shule ya kwa kuzingatia kuwa mbio hizo zinajumuisha watu wengi kutoka sehemu mbalimbali. Mgeni mashuhuri kwa mara nyingine alikuwa waziri wa maliasili na utalii Mh. Hamisi Kigwangala.
Wanafunzi wa kidato cha tano wakiwa darasani wakifuatilia somo la Computer Science kwenye Projector. Sekondari ya Eagles imeanzisha tahsusi mpya za PMCs, PCsG, na CBCs zenye somo jipya la Computer Science.