Eagles High School yapata tena matokeo mazuri ya mtihani wa kidato cha nne (CSEE 2022 EXAMINATION RESULTS)
Matokeo mazuri ya mtihani wa Form IV (CSEE** 2022 EXAMINATION RESULTS)
Uongozi wa shule ya Eagles High School unayo furaha kuwatangazia wananchi kuwa umepokea matokeo ya kufurahisha ya mtihani wa Form IV (NECTA CSEE Results 2022).
Kwa kifupi, baraza la mitihani la taifa (NECTA) limetoa matokeo ya kidato kidato cha nne mwaka 2022 yanayosomeka ifuatavyo:
Division I - wanafunzi 7
Division II - wanafunzi 12
Division III - wanafunzi 5
Division IV - wanafunzi 3
Division 0 - wanafunzi 0
Haya ni matokea mazuri na mafanikio makubwa kwa shule yetu, kwani jumla ya wanafunzi wote waliotahiniwa 27 wamefaulu. EXAMINATION CENTRE GPA 2.5376 GRADE B (VERY GOOD)
** Certificate of Secondary Education Examination (CSEE)
Download NECTA CSEE Results 2022 for S2354 EAGLES SECONDARY SCHOOL
APPLICATION FOR PRE- FORM V PROGRAM (12 WEEKS)
The Course runs for 12 weeks from 01/03/2021 to 31/5/2021. Though aimed at Boys who wish to join Eagles High School, it will also appeal to those waiting for their official NECTA results and possible Government placements later. We offer the course at TZS 500,000/=, refundable to those who join Eagles against their initial fees. We accept NECTA results so long as the Student has CDD in the chosen combination, but we reserve the right to suggest alternatives in consultation with the Parent.
Wanafunzi wa kidato cha kwanza wakifanya mtihani wao wa kwanza kwa kutumia tablet (E-Learning examination)
Wanafunzi hawa wamekuwa wakijifunza kwa njia ya mtandao (E-Learning) tangu mwanzoni mwa mwaka huu chini ya program inayoratibiwa kwa ushirikiano wa Opportunity Education na Vodacom Tanzania.
Mafunzo ya kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto
Hivi karibuni Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilitoa mafunzo ya kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto kwenye Shule ya Sekondari ya EAGLES. Kwa mara nyingine tena, hii ilikuwa nafasi nzuri na muhimu kwa wanafunzi na wafanyakazi wote kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na majukumu makubwa ya Jeshi hili ambayo ni kuokoa Maisha na Mali katika majanga mbalimbali.
Aidha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lilifanya pia ukaguzi wa Kinga na Tahadhari dhidi ya majanga ya moto, na kutoa ushauri wa aina na namna ya uwekaji wa vifaa vya kinga na tahadhari.
Mechi ya kirafiki kati ya wafanyakazi na wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita
Mechi ya kirafiki kati ya wafanyakazi na wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita (A- Level). Mechi kama hizi ni muhimu Sana katika kujenga mahusiano mazuri ya miongoni mwa jumuiya ya Eagles.
Eagles High School yapata tena matokeo mazuri ya mtihani wa Form VI (ACSEE 2020)
Uongozi wa shule ya Eagles Hiugh School unayo furaha kuwatangazia kuwa umepokea matokeo mazuri ya mtihani wa Form 6 (ACSEE 2020) uliofanyika Juni/Julai 2020.
Baraza la mitihani la Taifa ( NECTA) limetoa matokeo ya kidato kidato cha sita mwaka 2020 kama ifuatavyo:
Kwa kidato cha sita: ACSEE_results_s2354_2020.pdf
Div: I- 13
II- 39
III- 31
IV- 03
0- 01
Katika matokeo hayo mwanafunzi Godfrey Assenga kutoka Eagles aliyekuwa akisoma tahsusi ya ECA amekuwa ni miongoni mwa wavulana kumi (10) Bora kitaifa kwa masomo ya biashara huku akishikilia Nafasi ya nane (8).